MoroBuzz Season 3 Episode 1

Music: Fredrick Albert Komba Lyrics: Fredrick Albert Komba MoroBuzz Season 3 ep 1 lyrics
Piga Makofi
Piga nduru kama vile umekabwa Piga nduru kama tonge limekwama Demu ama jamaa akileta drama Sipotezi muda nashika tu simu block
Huu sio muda wa kutavutana Nina vitu vya kuvuta sio marijuana Nafanya nachopenda kwa bidii sana Nivute mikwanja nimpelekee Mama
Home wanasali nitusue Kidogo matofali nifyatue Wachawi wanataka wanipangue Kipindi Sir God amenipa duet
Piga makofi piga makofi, piga makofi tafadhali Piga makofi piga makofi, hata usipopiga mi sijali Piga makofi piga makofi, kama ndoto zako ni kufika mbali So upige makofi usipige makofi, makofi yako hayanikoseshi ugali
Mi napiga mishe nijaze matenga Studio kila siku najaza mabenga Nimebeba Bongo nzima kwa mabega Kipenzi cha watoto mpaka mabazenga
Wakati mna rehearsal kufanya playback Siku nikishika stage mtakuja learn kwamba Vile nitakavyopeleka hii climax Itabidi mrudi darasani mka learn kwanza
Nasoma kila siku ili nikue Mchezo nikiushika niubutue Siri nimeipata vipi niifichue? Bora kunyamaza acha niuchubue
Piga makofi piga makofi, piga makofi tafadhali Piga makofi piga makofi, hata usipopiga mi sijali Piga makofi piga makofi, kama ndoto zako ni kufika mbali So upige makofi usipige makofi, makofi yako hayanikoseshi ugali