Lyrics: PAUL THIMOS MWASILE/BONVENTURE ELIUTER KABOGO
Music: PAUL THIMOS MWASILE/BONVENTURE ELIUTER KABOGO
Intro
Yeeeeyehh/
Aaaah/
Toa ndugu/
Anakuona/
Verse 1
Eeh!kama nina nguvu ya kutafuta siwezi ita mtu Tajiri/
Tajiri sio kipaji ni kazi nguvu na akili/
Tatizo tukipata pesa tunapoteza marafiki/
Harafu tunapata wapambe ambao hatukuwa nao kwenye dhiki/
Neno la ufahamu ni lile neno lenye elimu/
Ila neno lenye utamu ni lile lililotiwa ndimu/
Japo wengi hawafahamu tofauti ya hamu na stimu/
Kama ilivyo tofauti ya maarifa na elimu/
Kipindi unamtongoza demu ili uonekane mjanja/
Mi namtongoza dalali ili nipate kiwanja/
Harafu sasa,ukipaka mkongo umkomoe mchumba/
Mwezako niko site ndio naipaka rangi nyumba/
Eeh!
Tusibishane kuhusu hili kuna vichwa viwili/
Ila cha chini hakifikiri/
Mwanume aliyevaa vikuku aliyetoga masikio na pua/
Huyo mwanaume sie hatuhusu sio mwanaume tunaemjua/
Maskini wenge tuna ndoto za utajiri kichizi/
Hazitimii sababu tunastuka katikati ya usingizi /
Hatujakuzwa kuamshwa na alarm ili tuamke/
Tunaamshwagwa na shida Tuache shuka tukatafute/
Chorus
Toa ndugu ,toaaaa(toa ndugu)
Toa ulicho nacho (ulicho nacho)
Bwana anakuona(anakuona)
Mpaka moyoni mwako x2
Verse 2
Acha nikwambie/
Kuna urithi wa aina mbili/
Kuna urithi wa mali na ule urithi wa akili/
Urithi wa mali,utakupa mali za utajili/
Ila urithi wa akili unaweza usikupe akili za dili/
Na kwenye Maisha/
Maisha hayaishi sababu yako
Ila wewe ndio unasababu ya kuishi kivyako /
So kabla ya kuvuta ganja hakikisha unavuta pumzi/
Maana pesa ni mwanamke ambae abaki kama umtunzi/
Na kwenye ukoo sina ndugu yeyote Tajiri/
Na kama yupo basi lazima awe mbahiri/
Mungu anables adoado najikongoja/
Na ghetto nikiishiwa gesi nawasha data naunga mboga/
Mama angu pekee ndiyo mwanamke nae mwamini/
Japo nae alirubuniwa ndiyo nikapatikana mimi/
Peace kwa wanawake wote kima cha chini na juu/
Nawapa mimba za fikra msimeze p2/
Mambo madogodogo hayo nitawapa haina kwele/
Siwezi kuwapa nyumba labda nyumba za milele/
Na kuhusu kupush mtapush mkipata mimba/
Kwa hiyo ni udhushi nikisema mtapush ndinga/
Chorus
Toa ndugu ,toaaaa(toa ndugu)
Toa ulicho nacho (ulicho nacho)
Bwana anakuona(anakuona)
Mpaka moyoni mwako x2
Hook
Usifanye moyo wako kuwa mgumuu weweβ¦..
Toa ulicho nacho huende bwana anakuonaβ¦.