Lyrics: Goodluck Gozbert/Timothy Boikwa
Music: Goodluck Gozbert/Timothy Boikwa
Nimeona Majina Makubwa,
kupita Yote Ila katika Hayo langu lilikua juu
Nimeona Magari mazuri ya dunia hii
Tena katika hayo langu Lilikuwa Juu
Nikaona Yaliyo mafanikio nyingi Baraka
Tena katika hizo zangu zilikua
Wacha nikueleze patano langu na Mungu
Napitishwa hapa Ananipeleka Juu
Ukionaninapumua bado
Misuko suko ni kama zoezi
Sichanganywi na Ripoti ya Leo
Mchicha Bamia sio
Sukuma wiki Najizungusha nikingojea Nyama
Bado Sijakamilika
Ninatayarishwa
Ukiweza Nihukumu nikiwa na hali ngumu
Ila ungalijua ungekaa kimya
Alinipaka mafuta nitawale
Nami nasubiri Baraka zangu niketi enzini
Sawa Nimezidi mikopo madeni ya kila duka
Hao ni maajenti wa Kampuni Yangu Ya Baadae
Ninabariki wenzangu Maana Nimebarikiwa
Sina laana Kwanini Niwachukie Eh
Ninaombea wenzangu Wafanikiwe Wajue,
Ndivyo Tulivyo washindi
Wacha nikueleze patano langu na Mungu
Napitishwa hapa Ananipeleka Juu
Ukionaninapumua bado
Misuko suko ni kama zoezi
Sichanganywi na Ripoti ya Leo
Mchicha Bamia sio
Sukuma wiki Najizungusha nikingojea Nyama
Bado Sijakamilika, Ninatayarishwa