Music: Abisay hizza Lyrics: Abisay hizza Story ya maisha yangu kwa kifupi mi nakupa Jinsi ilivyokuwa huu wokovu nikapata Sio mpango wa mungu watu wengi wanahisi Kumleta mrembo malkia sio rahisi Sikiliza nikusumbue ilivyokuwa ndugu yangu Siku moja maskani nimechill na wanangu Alipita mrembo mnyamwezi nikaunga tela Nikaanza kumsemesha huku nikimwaga sera Kanikatia juu juu na hilo jibu shindwa Sikukata tama kesho yake nikadamka Nikaanza fuatilia wapi anatokea wapi anaelekea Nilikata tamaa nilipoona kanisani kivipi niwe naye Na yeye ni msafi kwanzia matendo sura mpaka tabia Kichwa chini nikaondoka huku nikimfikiria.
Nawaza kwa kina juu ni upendo Wa namna gani Utafanya chochote ili mimi Nikuamini Ivi upendo maana yake ni nini? Mungu anajua maana yake ni nini
Utata unakuja usiku nikilala ni yeye namuotea Yu karibu nami na ni tenzi ananiambia Mara ananiombea mara ananiambia Yesu anaokoa Stori za biblia ndugu yangu ndio usipime Story ya mwisho ilikuwa ya paulo mtume Jumapili nakurupuka kanisani najiandaa Majamaa wanashangaa nilivyovaa Suruali ya kitambaa nimepasi imenyooka Chini mepiga moka ndio mtoko niliotoka Kanisani siti ya mbele karibu na wanakwaya Lengo langu aninone ye sianaimbaga kwaya Hazikupita week mbili nikajiunga na kwaya Taratibu taratibu injili nikaipokea Sikuamini mimi kama yesu ningempokea Mungu wa ajabu.
Ivi upendo maana yake ni nini? Mungu anajua maana yake ni nini Ivi upendo maana yake ni nini? Mungu anajua maana yake ni nini
Amini usiamini mungu anakupenda Hivyo atatumia njia yeyote ili kukuokoa Na ukiamini chochote kinaweza kuwa.